

Lugha Nyingine
车主注意!20日零时起白云机场免费停车时段有调整
ALMATY - Shirika la ndege la China limezindua njia ya usafiri wa ndege wa moja kwa moja kati ya Beijing, China na Almaty, Kazakhstan jana Jumatano, na kufanya hafla ya usafiri wa kwanza wa ndege kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Almaty. Ndege CA799 na CA800 zitatoa huduma hiyo mpya ya usafiri wa kwenda na kurudi kila Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili kwa kutumia ndege ya Boeing 737.
Chen Zhaozhen, meneja mkuu wa Shirika la Ndege la China, Tawi la Almaty amesema, njia hiyo mpya ya usafiri wa ndege itakuwa kama daraja la anga kati ya miji hiyo miwili, na njia hiyo inatarajiwa kuinua ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara, mawasiliano ya kiutamaduni na utalii kati ya China na Kazakhstan kwenye kiwango kipya. Galiya Toxeitova, mkuu wa Idara ya Utalii ya mji wa Almaty, ameelezea imani yake kwamba njia hiyo mpya italeta urahisi zaidi kwa usafiri kati ya nchi hizo mbili.
Kwa kutazama siku za baadaye, ameelezea matumaini ya kupanua ushirikiano na kuongeza usafiri wa ndege wa moja kwa moja, ili kuleta manufaa zaidi kwa wasafiri na kuingiza msukumo mpya katika maendeleo ya uchumi wa kikanda.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma